Shahidi: Tundu Lissu hakuhusika katika kuandaa mkutano na wanahabari

Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu, inaendelea katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Waandishi wa BBC Swahili

  1. Lissu: Waeleze majajji nani aliyeamua huo mkutano ufanyike

    .
    Maelezo ya picha, Tundu Lissu

    Brenda ni shahidi mwengine wa upande wa Tundu Lissu

    Lissu: Nje ya hizi nafasi za kichama wewe ni nani

    Brenda: Mimi nimesomea Bachelor of science in Accounting Gloucestershire University nchni Uingereza kuanzia mwaka 2009 hadi mwaka 2013

    Lissu: Waeleze majaji Tuzo au awards uliyoipata baada ya kusoma huko

    Brenda: Nilipata Cheti baada ya kuhitimu

    Lissu: Waeleze majaji utaalamu wako mwingine kama upo

    Brenda: Hapana hakuna

    Lissu: Waeleze majaji uzoefu wako wa kazi za kitaaluma nje ya kazi za kisiasa

    Brenda: Kwa mwaka mmoja baada ya kuhitimu nilifanya kazi kwa mwaka mmoja na baadae nikaanza kufanya biashara za kawaida

    Lissu: Waeleze majaji ulifanya kazi gani wapi na mwaka gani

    Brenda: Niliajiriwa kama accountant TAZ Cars nilifanya kwa mwaka mmoja nikaanza kufanya biashara Kariakoo

    Lissu: Ulifanya kazi kwenye hiyo kampuni toka lini hadi lini

    Brenda: Nilipohitimu mwaka 2013 niliajiriwa mpaka mwaka 2015 na baada ya hapo nikaanza kufanya biashara ya nywele na urembo wa wanawake Kariakoo na baadaye nikaanza kuuza vifaa vya umeme

    Lissu: Ukisema uliuza urembo una maaana gani?

    Brenda: Nilikuwa nauza vifaa vya urembo

    Lissu: Sasa shahidi baada ya kutupa historia yako kwa ufupi naomba tuzungumzie kesi ambayo unaitolea ushahidi leo hii. Swali langu la kwanza kuhusiana na hii kesi waeleze majaji ufahamu wako juu ya mkutano wa tarehe tatu April 2025

    Brenda: Waheshimiwa majaji Chama kilialika watia nia makao makuu ya chama mikocheni kuja kuzungumzia kuhusiana na msimamo wa ‘No reforms no election’

    Lissu: Waeleeze majaji hao watia nia ni watu gani

    Brenda: Ni wale waliokuwa na nia kugombea chaguzi za kiserikali 2025

    Lissu: Waeleze majaji hiyo uliyokuja kuzungumzia ‘No reforms no election ni nini

    Brenda: Ni msimamo wa chama ulioelekeza bila mabadiliko hakuna uchaguzi mabadiliko ya sheria za kiuchaguzi

    Lissu: Waeleze majajji nani aliyeamua huo mkutano ufanyike

    Brenda: Ni katibu mkuu wa chama na sekretarieti

    Lissu: Katibu mkuu ni nani?

    Brenda: Waheshimiwa majaji katibu mkuu anaitwa John Mnyika

    Lissu: Unaposema sekretarieti una maana gani shahidi

    Brenda: Ni chombo cha utekelezaji wa kazi za chama za kila siku

    Lissu: Hiki chombo kina wajumuisha wakina nani?

    Brenda: Waheshimiwa majaji hiki chombo kinaundwa na katibu mkuu na manaibu wake wawili wa bara na Zanzibar Mkurugenzi wa chama

    Lissu: Hao manaibu katibu hawana majina

    Brenda: Mmoja anaitwa Amani Golugwa bara na wa Zanzibar anaitwa Ally Ibrahim

    Wakurgenzi ni Brenda Rupia mkurugenzi mawasiliano na uenezi, John Kitoka mkurugenzi mambo ya nje, Mkurugenzi wa Fedha Tito Kitalika, Mkurugenzi wa operesheni na uchaguzi John Pambalu, Mtaalamu wa rasilimali Lenard Magere, Makatibu wa mabaraza , Baraza la wazee Hellen Kayanza, Baraza la wanawake Pamela Maasai, Baraza la vijana Dua Lyamzito, Mkurugenzi wa sheria Gaston Galubindi.

    Lissu: Waeleze majaji huo mkutano wa sekretarieti ulifanyika lini?

    Brenda: Sikumbuki tarehe ya kikao tulichofanya ili kuitisha huo mkutano

    Lissu: Sasa waeleze waheshimiwa majaji kikao hicho kiliamua nini kifanyike

    Brenda: Waheshimiwa majaji kikao hicho kiliamua kwamba tutoe taarifa kwa watia nia kwenye huo mkutano na kwamba Chadema itakuwa na watia nia kwenye huo mkutano

    Lissu: Baada ya kuamua watia nia wafahamishe na umma ufahmishwe kitu gani kilifanyika

    Brenda: Mkurugenzi wa mawasiliano aliandika ujumbe kwa umma tarehe 27/03/2025 kuujulisha umma kutakuwa na mkutano na watia nia tarehe tatu April na kuwataka watia nia wafike ofisi za chama kwa ajili ya mkutano huo na chama.

    Lissu: Nini kilifuata

    Brenda: Tuliweka kwenye kurasa za mitandao ya kijamii baada ya kuwa nimeandika kwa kurugenzi yangu ya mawasiliano ambayo ilitoa taarifa juu ya mkutano huo kwa vyombo vya habari na nikavialika

    Lissu: Naomba urudie tena

    Brenda: Niliandika barua nikaweka kwenye kurasa za mitandao ya kijamii za Chama, Kisha nikaalika vyombo vya habari

    Lissu: Sasa mimi nimeshitakiwa na nimekuwa gerezani nikituhumiwa mimi ndiye niliyealika vyombo vya Habari, wewe unasemaje?

    Brenda: Waheshimiwa majaji Mheshimiwa Tundu Lissu sio yeye aliyeandaa mkutano na watia nia wala kualika vyombo vya habari

    Lissu: Waeleze majaji kwenye mwaliko wa waandishi wa habari iwapo kulikuwa na maelekezo yoyote waje na nini na waje wafanye kazi yao vipi

    Brenda: Tunapowaalika waandishi wa habari hatuwapi maelekezo yoyotewanakuja kufanya kazi yao kwa utaalamu wao, na tuliwaalika waje wachukue taarifa ya watia nia na chama

    Lissu: Waeleze majaji siku ya mkutano watu gani walihudhuria mkutano huo

    Brenda: Waheshimiwa majaji watia nia walihudhuria, wajumbe wa sekretarieti pamoja na viongozi wakuu wa Chama

    Lissu: Viongozi wakuu wa chama ni akina nani

    Brenda: Viongozi wakuu wa chama ni Manaibu makatibu wakuu wawili Aman Golugwa na Ally Ibrahim, Makamu mwenyekiti Zanzibar Said Mzee Makamu, mwenyekiti Bara Mheshimiwa John Heche na Mwenyekiti Taifa Mheshimiwa Tundu Antipas Lissu na katibu mkuu wa Chama Mheshimiwa John Mnyika.

    Lissu: Watu gani wengine walikuepo?

    Brenda: Walikuepo watia nia wa sekretarieti pamoja na waandishi wa habari

    Lissu: Ulikuwa na wastani wa watu wangapi?

    Brenda: Takribani watu 250

    Lissu: Waeleze majaji kimahususi kuhusiana na waandishi wa habari waliokuja ni wa vyombo gani vya habari

    Brenda: Waandishi waliokuja ni pamoja na Chanzo TV Mwanzo TV, Jambo TV, ITV na vyombo vingine vya online ikiwemo Mwananchi, hao ndio ninaowakumbuka

    Lissu: Walikuja vipi?

    Brenda: Waheshimiwa majaji walikuja na kamera na vipaza sauti na wengine kalamu na karatasi

    Lissu: Sasa ushahidi umeletwa mahakamani, kati ya hao waandishi wa habari waliokuja, wapo waliorusha matangazo ya mkutano huo moja kwa moja waeleze majaji moja kwa moja

    Brenda: Ni ngumu kesema kama walirusha au hawakurusha sababu kuna wanaorekodi na kurusha baadaye na kuna ambao hawatarusha kabisa

    Lissu: Kuna taarifa kwamba Jambo TV walirusha Taarifa hiyo moja kwa moja, wewe unasemaje?

    Brenda: Waheshimiwa majaji ni ngumu kusema sababu hatuwapangii namna ya kufanya kazi

    Lissu: Wewe ulikuwepo kwenye huo mkutano uliona wakifanyaje kazi?

    Brenda: Waheshimiwa majaji, waandishi walikuwepo ila ni ngumu kusema kama walirusha matangazo moja kwa moja au la au hata kama walirekodi sababu walikuwa tu kwenye huo mkutano

    Lissu: Kwa kuwa mimi ndio mshitakiwa waeleze majaji mimi nilifanya nini kwenye mkutano huo

    Brenda: Mwenyekiti alikuwa mzungumzaji pamoja viongozi wengine wa chama

    Lissu: Nilikuwa mzungumzaji wa aina gani?

    Brenda: Hapana ulikuwa mzungumzaji mwalikwa na ulitoa hotuba kama mwenyekiti wa chama na ndio alikuwa mzungumzaji mkuu

    Lissu: Waeleze majaji kitu kingine chochote ulichokiona mwenyekiti akifanya zaidi ya kuwa mzungumzaji mkuu

    Brenda: Sikuona kitu kingine chochote mwenyekiti alichokifanya zaidi ya kuwa mzungumzaji mkuu

    Lissu: Ushahdi uliopo unasema mimi ndiye niliyetayarisha hayo matangazo na kuyaweka mitandaoni hususan jambo tv wewe unasemaje?

    Brenda: Waheshimiwa majaji hayo yatakuwa mashitaka ya uongo na wala sio mfanyakazi wa jambo tv hayo ni mashitaka ya uongo na wala alikuwa hafahamu kama Jambo tv watakuepo kwenye huo mkutano

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji Nzengelei waheshimiwa majaji tunaona muda umekwisha tunaomba muongozo wa mahakama kama shauri linaweza kuahirishwa

    Jaji: Tuendelee kidogo

    Lissu: Ahsante waheshimiwa nimalizie hili. Shahidi swali langu lilikuwa mwenyekiti hakuwa anajua juu ya uwepo wa jambo TV waeleze majaji mwenyekiti kufahamu kama anajua waandishi wa habari walikuwa wamealikwa

    Brenda: Sinadhani kama alikuwa anafahamu, sababu ni kazi yangu mimi na kurugenzi ya mawasiliano

    Lissu: Swali langu la mwisho kwa leo nani ni mmiliki wa hayo matangazo au hiyo Taarifa.

    Brenda: Ni Mmiliki wa chombo husika

    Lissu: Waeleze majaji kuhusu Taarifa iliopeperushwa na Jambo tv April tatu mwaka jana

    Brenda: Waheshimiwa majaji mmiliki wa taarifa ya Jambo TV ni jambo TV wenyewe au mkurugenzi wa Jambo TV

    Jaji: Shauri linaahirishwa mpaka kesho saa tatu asubuhi

  2. Lissu amuhoji Mkurugenzi wa Mawasiliano CHADEMA

    .
    Maelezo ya picha, Tundu Antipas LIssu

    Lissu: Shahidi wangu namba nne anaitwa Brenda Jonas Rupia

    Jaji: Shahidi unaitwa nani?

    Brenda: Naitwa Brenda Jonas Rupia Mkurugenzi wa Mawasiliano na uenezi CHADEMA

    Shahidi anakula kiapo

    Lissu: Umesema unaishi Basihaya kata ya Bunju iko wapi?

    Brenda: Waheshimiwa majaji Basiaya iko ndani ya jimbo la Kawe wilaya ya Kindondoni Mkoa wa Dar es salaam

    Lissu: Umewaeleza majaji wewe ni mkurugenzi wa mawasiliano na uenezi CHADEMA hii kazi umefanya tangu lini?

    Brenda: Kuanzia tarehe 12/3/2025 nilipoteuliwa na kamati kuu ya chama

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kabla ya hiyo tarehe ulikuwa na nafasi gani ndani ya Chama

    Brenda: Nilikuwa katibu wa Bawacha Mkoa wa kichama Kindondoni

    Lissu: Waeleze majaji Bawacha ni nini

    Brenda: Waheshimiwa majaji Bawacha ni Baraza la wanawake CHADEMA

    Lissu: Hiyo nafasi ya Bawacha ulishapata hiyo nafasi tangu lini?

    Brenda: Nilishika nafasi hiyo kwa mwaka mmoja nikiteuliwa mwaka 2024

    Lissu: Waeleze majaji nafasi nyingine uliyokuwa nayo ulipochaguliwa Kinondoni

    Brenda: Nimekuwa mwenyekiti CHADEMA kata ya Mwananyamala na baadaye nikachaguliwa mwenyekiti wa Bawacha jimbo la kinondoni vyote hivyo ni kati ya 2015 na 2024

  3. Shahidi anayefuata ni Brenda Rupia

    Mahakama imerejea

  4. Shahidi: Ilikuwa haki yetu kushiriki uchaguzi huru na wa haki lakini tulizuiliwa

    Lissu: Sasa shahidi nilisema ilikuwa haki yetu kutoshiriki uchaguzi ila tulizuiliwa na tume ya uchaguzi hebu fafanua

    Shahidi: Ni kweli ilikuwa haki yetu kushiriki uchaguzi huru na wa haki lakini tulizuiliwa na tume ya uchaguzi

    Lissu: Unakumbuka kutoa ushahidi kuhusiana na kuenguliwa kwa wagombea wa CHADEMA ukasema hujawahi kuona uchaguzi wowote huru ulioendeshwa na Tume ya Uchaguzi ukaulizwa kama CCM walisema wagombea wao wameenguliwa fafanua

    Shahidi: Taarifa za wagombea kuenguliwa zinakuweko kwenye ofisi za taasisi na sijawahi pokea taarifa yoyote kutoka Chama cha Mapinduzi

    Lissu: Uliulizwa juu ya usahihi wa mahesabu yako juu ya matokeo ya rais ukasema asilimia 98.6 zilienda kwa Samia ukasema asilimia mbili nukta nne zilienda kwa wengine. Ulipoulizwa kama unajua hesabu ulisema hiyo ni human error ulikuwa na maana gani?

    Shahidi: Waheshimiwa ……

    Jaji: Si ni human error aseme nini kingine

    Lissu: Inatosha hiyo kaka

    Shahidi: Inatosha

    Lissu: Uliulizwa kama maandamano huleta bugudha kwa watu ukasema maandamno huleta bugudha kwa watu fulani hebu fafanua jibu lako

    Shahidi: Ni kweli inaleta bugudha kwa watu mbali mbali, huwa ni bugudha inayowasha masikio na macho. Utaratibu wa siku huwa unabugudhika kwenye barabara

    Lissu: Shahidi uliulizwa maswali mengi kuhusu uhuru wa Tanzania ukasema ndio na mahakama hazitakiwi kuingiliwa na taasisi nyingine za nje. Ukaulizwa kama zinaweza kuelekezwa na EU lakini mamlaka nyingine zinaweza zungumzia maswala ya ndani ya Tanzania ikiwepo masuala yaliyoko mahakamani ulikuwa na maana gani?

    Shahidi: Tanzania sio kisiwa kama nchi ina wajibu wa kuzingatia matamko ya kidunia yanayohusiana na haki za binadamu inawajibika kuheshimu sheria za kimataifa

    Wakili: Huu ni ushahidi mpya waheshimiwa majaji naona wanaanza kuleta mambo mapya waheshimiwa majaji

    Lissu: Ulisema mtu mmoja peke yake hawezi akafanya kosa la uhaini fafanua

    Shahidi: Nilichomaanisha mshitakiwa hawezi kutenda kosa la uhaini peke yake kwamba amepanga yeye akachochea baada ya kujichochea na kufanya hilo kosa mwenyewe

    Lissu: Uliulizwa juu ya uhuru wa tume na ukasema huo uhuru wa tume haupo sababu huo uteuzi umelenga kuweka udhibiti kwa mtu mmoja ulikuwa na maana gani

    Shahidi: Uteuzi huwa unafanywa na mtu mmoja ambaye ni rais na wale aliowateua na kwamba wanampa yeye kipaumbele

    Lissu: Uliulizwa mwaliko kwa Naibu Katibu Mkuu Zanzibar ilikuwaje umualike wakati yeye ni sehemu ya kamati ya maandalizi na ukasema ilikuwa tu nia njema sababu anaishi Zanzibar

    Shahidi: Waheshimiwa majaji

    Jaji: Unamajibu tofauti

    Shahidi: Ni hayo hayo tu waheshimiwa majaji

    Lissu: Unakumbuka uliulizwa maswali mengi kuhusina na mkutano wa Aprili ulinikatisha kwenye mkutano ila hukuniandikia hotuba wala hukunipa hotuba ila ulijua nini kiko kwenye fikra zangu ziku hiyo

    Shahidi: Nilichomaanisha ni kwamba sekretariet inapoandaa mkutano nilikuwa ninajua tunazungumzia swala la ‘no reforms no election’

    Lissu: Uliulizwa juu ya mikutano ambayo mimi na wewe tulifanya na wadau mbalimbali, uliulizwa mkutano wetu na Shura ya Maimam, ukaulizwa kama yale maneno ya kuzuia uchaguzi kama niliyasema, ukaulizwa kama nilisema kukinukisha kwa Warioba na punde ukasema sikusema ukaulizwa huoni unatoa ushahidi wa uongo ulikuwa na maana gani

    Shahidi: Nilikuwa namaanisha ni hali ya kawaida ya mtiririko wa mazungumzo, muktadha wa jambo la msingi huwa linasema kwa hiyo hilo neno moja kukosekana halikuondoa maana ya ujumbe husika kufikishwa

    Lissu: Leo umeulizwa na Katuga zile rekodi zinazochukuliwa na chombo cha habari ni mali ya chombo husika ukasema ni mali yake kwa chombo husika ukaulizwa useme kifungu ukasema hujui hebu fafanua

    Shahidi: Kwa ninavyofahamu anayerekodi ndiye mwenye kile kinachorekodiwa sababu yeye amekuja na vifaa vyake

    Lissu: Umeulizwa nilisema majaji ni Ma-CCM ukasema hukumbuki na ukaulizwa kama nikisema mahakamani hakuendeki na mapolisi wanaingiza kura kwa vibegi. ukasema hukumbuki ulimanisha nini?

    Shahidi: Nilimaanisha kile nilichokisema kilitokana na kile nilichokisikia

    Lissu: Uliulizwa juu ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana ukasema kweli kulikuwa na vurugu ukasema jumuiya ya Ulaya ilisikitishwa na vurugu hizo na ukasema sio kweli kwamba Lissu ndio alisababisha vurugu sababu alikuwa gerezani

    Shahidi: Nilichokuwa namaanisha hapo baada ya CHADEMA kuzuiwa kufanya shughuli zake haikujihusisha na siasa tena na mwenyekiti alikuwa gerezani na sio kweli kwamba vurugu zilizotokea zililetwa na CHADEMA au nini

    Lissu: Uliulizwa kuhusu hotuba ya jaji Chande ukasema ulisikiliza sehemu sehemu ukasema alisema vurugu za Oktoba zilipangwa ukasema hukumbuki. Ukaulizwa uchaguzi kuvurugika ukasema uchaguzi ukivurugika na ukasema walioko madarakani wanaendelea ulikuwa na maana gani?

    Shahidi: Waheshimiwa majaji nilikuwa na maana mbili katiba yetu inatupa fursa ya kusogeza chaguzi mbele kukiwa na changamoto maana ya pili ni maana iliyoko katika msimamo huu ya kwamba tuko tayari. CHADEMA ilikuwa tayari na iko tayari hata ingebidi uchaguzi kusogezwa mbele ili kupata mabadiliko kwenye mifumo ya uchaguzi

    Lissu: Uliulizwa kuhusu kuhamasisha uasi ulisema yanapaswa kutafsiriwa kwa muktadha wake na yangewatia wasiwasi una maana gani?

    Shahidi: Nilimaanisha mkutano huo wa watia nia walielimishwa kwa kuoneshwa sheria ambazo tunazo na ni mbovu na zinatakiwa kufanyiwa mabadiliko na neno uasi nilimaanisha tutakwenda kinyume na sheria mbovu ili kupata sheria nzuri.

    Waheshimiwa zile dakika nilizoomba zimebaki ngapi

    Jaji: Tumeongeza

    Shahidi: Kama nimeongeza samahani waheshimiwa majaji Ahsanteni sana. Nimemaliza waheshimiwa majaji

    Jaji: Shahidi umemaliza kutoa ushahudi wako mahakama inakuruhusu

    Tunakwenda mapumziko hadi saa tisa

  5. 'Unafahamu mshtakiwa anashtakiwa kwa kuvuruga uchaguzi'?

    Wakili: Ni ushahidi wako unasema Jumuiya ya Ulaya walisikitishwa na vurugu siku ya uchaguzi

    Shahid: Ni kweli.

    Wakili: Na pia Mwenyekiti alisema kuwa huu uchaguzi tunakwenda Kuuvuruga

    Shahidi: Ndio

    Wakili: Waambie majaji ni kweli au Sio kweli Siku ya Uchaguzi kulikiwa na Vurugu

    Shahidi: Ni kweli kulikuwa na vurugu

    Wakili: Nitakuwa sahihi nikisema kile mwenyekiti alichosema kuwa Watavuruga Uchaguzi na kweli Vurugu Zikatokea kwa mujibu wa hotuba ya Mwenyekiti ni kweli au sio kweli kwamba kilichopangwa kwa vurugu kilitumia vurugu zilizotokea

    Shahidi: Sio kweli

    Wakili: Unajua au hujui ni aina gani ya Uhaini ambayo ameshtakiwa nayo mshtakiwa unayemtetea

    Shahidi: Hafahamu

    Wakili: Je unafahamu au haufahamu mwenyekiti anashtakiwa na aina gani ya shtaka la Uhaini?.

    Shahidi.

    Wakili: Unafahamu au haufahamu kwamba mshtakiwa anashtakiwa kwa kuchapisha na kutoa maneno ya Kuvuruga Uchaguzi. Tunakwenda kuzuia huu Uchaguzi na Tunakwenda kukinukisha

    Shahidi: Anafahamu

    Wakili: Kwa Mujibu wa ushahidi wako ni kweli au sio kwelikwamba mshtakiwa ametoa hayo maneno

    Shahidi: Mshtakiwa alitoa hotuba ndefu yenye hayo maneno

    Wakili: Waambie majaji katika mkutano wa April 3 mwaka 2025 baada ya malalamiko ya upungufu katika Uchaguzi. Mshtakiwa au Mwenyekiti alikuja na alitangaza maadhimio yenye Senstesi Chache zenye nguvu Kwamba Tunaenda Kuzuia Uchaguzi

    Shahidi: Hawakuwa na kikao chenye maazimio.

    Wakili: Baada ya Mwenyekiti kusema majaji ni Maccmmahakamani hakuendeki Kilichobaki tuende tukavuruge Uchaguzi na tukazuie Uchaguzi na tunakwenda Kukinukisha ni kweli au sio wajumbe walicheka na kushangilia

    Shahidi: Hakumbuki

    Wakili: Umesema kuwa uchaguzi upo kwa mujibu wa sheria na sio haki kumzuia mtu.. je kulikuwa na nia yoyote ya Mwenyekiti Kufungua Kesi mahakamani Kupinga Uchaguzi

    Shahidi: Hakukuwa na nia ya kufungua kesi kuzuia Uchaguzi bali ilikiwa nia ya kuelimisha

    Wakili:Je wambie majaji kama ulisema katika Ushahidi wakoMwenyekiti aliwapa katika hotuba yake njia ya kuzuia Uchaguzi

    Wakili: Huyu unayemzunguzia amesema maneno ‘majaji ni Maccm’ anasema Kayasema kwenye mkutano Je, unakubaliana naye?

    Shahidi: Hajawahi kuyasikia hayo maneno

    Wakili: Waambie majaji kama vikao vya chama chenu huwa vinakuwa na maazimio

    Shahidi: Katika utaratibu wa kawaida vikao vinakuwa na Maazimio

  6. 'Ni kweli au sio kweli kwamba neno kukinukisha ni kitendo'?

    .
    Maelezo ya picha, Tundu Lissu

    Wakili: Waambie majaji ni kweli au sio kweli katika uandishi wa kumbukumbuku za maazimio ni yenye sentesi fupi zenye kueleweka.

    Shahidi: Ni kweli

    Wakili: Neno kukinukisha uliliskia?.

    Shahidi: Ndio nilisikia.

    Wakili: Ni kweli au sio kweli kwamba neno kukinukisha ni kitendo

    Shahidi:. Ni kitendo

    Wakili: Katika ushahidi wako ulioeleza mahakama ni kitendo gani kilisemwa na mwenyekiti ili kukinukisha kufanyike

    Shahidi: Hakusema kitendo bali alitoa tafsiri ya neno kukinukisha

    Wakili: Waambie majaji ukichoma kitu ikiwemo matairi yanatoa au hayatoi harufu

    Shahid: Hakumbuki

    Wakili: Je mwenyekiti siku ya hotuba yake alieleza njia ambayo itatumika kukinukisha katika Uchaguzi Mkuu...

    Shahidi: Haikueleza hiyo dhamira.

    Wakili: Inawezekana watu waliambiwa kama mashabiki wa simba wakachimbe Jangwani dawa

    Shahidi:…

    Wakili: Ni haki au sio haki kwa mtu yeyote aliyepo kusikiliza hotuba ya Lissu na kutafsiri yale maneno kwa jinsi anavyojua yeye

    Shahidi: Siwezi jisemea.

    Wakili: Kwa kuwa njia ya kukinukisha haikuwa imefafanuliwa nitakuwa sahihi nikisema ni haki ya mtu akiamua kwenda kujisaidia kwenye kituo cha kupiga kura na kuacha dude lake pale linanuka.

    Shahidi: Sio Haki

    Wakili: Waambie majaji ni haki au sio haki kwa hiyo mtoaji wa hiyo hotuba kwenda kufanya vituo vya kupiga Kura vinuke kwa kuchoma moto

  7. ''Sentensi 'Tunaenda kuzuia uchaguzi' ni kamilifu na yenye maana?''

    Wakili: Waambie majaji iwapo sentensi TUNAENDA KUZUIA UCHAGUZI ni kamilifu na yenye maana au sio kamilifu isiyo na maana

    Shahidi: Ni kamilifu na ina maana

    Wakili: Unaenda kuvuruga uchaguzi Je, ni Kamilifu na inayotoa maana au sio kamilifu na isiyoleta maana.

    Shahidi: Ni kamilifu ukisoma yote

    Wakili: Ulirejelea hotuba ya mwenyekiti ya Aprili 3, ulirejelea maneno mengi sana na uliwaambia majaji kuwa kilichoandikwa kwenye hati ya mashtaka ni kisehemu kidogo chenye sekunde 26. Sasa waambie majaji kwenye hiyo hotuba kama ulisikia kweli, je ulimsikia mwenyekiti akisema kwamba majaji ni MACCM?

    Shahidi: Hakumbuki.

    Wakili: Je ulisikia mahakamani hakuendeki

    Shahidi: Hakumbuki

    Wakili: Je, ulisikia mwenyekiti akisema kuwa mapolisi wanaingiza kura feki kwenye vibegi vya mgongoni

    Shahidi: Hakumbuki

    Wakili: Wewe yale uliyoyasema ukirejea maneno ya mwenyekiti kwenye mkutano wa mwenyekiti wa Aprili 3 mwaka 2025 umeyasema yote au machache kati ya mengi aliyoyasema

    Shahidi: Nimesema yale katika yote aliyoyasikia yeye.

    Wakili: Je, hujui au unajua kama yapo maneno mengine ambayo alisema ambayo wewe huyajui.

    Shahidi: Sifahamu

    Wakili: Je yale uliyoyasema hapa mahakamani yamechukua Lisaa moja na Nusu au yamechukua Dakika Chache

    Shahidi: Yale ambayo ameyasema

  8. Shahidi Aman Golugwa anaendelea kuhojiwa

    KATUGA.

    Wakili: Waambie majaji ni kwelii kwamba aliwaambia vile vitu vilivyochukuliwa na mwandishi wa habari ni mali yake na anaweza kutumia atakavyo

    Shahidi: Ni kweli

    Wakili: Hayo maneno ni kwa mujibu wa sheria au kwa mujibu wa maoni yako

    Shahidi: Ni kwa mujibu wa sheri na uelewa wake

    Wakili:Je, umetaja sheria gani, je katika ushahidi wako umeitaja Sheria Mahususi

    Shahidi: Ni mali yake na kwamba hajataja Sheria.

    Wakili: Ni kweli kuwa nilikusikia kwamba uliwaambia Majaji kuhamasisha uasi sio kosa kisheri ni neno La kisiasa Je, unakumbuka ulisema haya maneno?

    Shahidi: Ndio nakumbuka kuyasema

    Wakili: Je, siasa mnazofanya mnatumia lugha gani

    Shahidi: Lugha ya Kiswahili.

    Wakili: Kamusi gani inayotumika kutafsiri hiyo Lugha ya Kiswahili

    Shahidi: Wanatumia kamusi ya Kiswahili kutafsiri.

    Wakili: Je, kwa ufahamu wako kuna kamusi inayoitwa kamusi ya Lugha ya Kisiasa.

    Shahidi: Hakuna kamusi ya Lugha ya kisiasa

    Wakili: Ulikuwa unarejeshwa kwenye maneno ya hati ya mashtaka ulisema kwa ufahamu wake unaotokana na uzoefu wa siasa hakuna kosa lolote mtu akisema anaenda kuvuruga Uchaguzi hii ni kwa mujibu wa sheria au uzoefu wako?

    Shahidi: Sio maoni ni kweli kwa shughuli za Kisiasa

    Wakili: Je, unajua au hujui kuwa uchaguzi mkuu upo kwa mjibu wa katiba

    Shahidi: Anafahamu kuwa uchaguzi Mkuu wa Wabunge madiwani na Rais upo kwa mujibu wa katiba

    Wakili: Ulimwambia jaji kwa ufahamu wako kwamba kitendo cha kuvunja sheria hakikupeleki kuwa na kosa la Uhaini

    Shahadi: Hadi akumbuke

    Wakili: Ulisema kitendo cha kupinga sio kosa je, Ulitaja Sheria

    Shahidi: Kupinga sio kosa ila sikutaja Sheria.

  9. Natumai hujambo na karibu tena katika muendelezo wa habari za moja kwa moja kutoka mahakamani

  10. Katuga kwa Golugwa- Ulisema mpaka mshinikize mabadiliko mumshinikize nani?

    Katuga: Wewe ni miongoni mwa watu wanaotaka katiba ya nchi ibadilishwe unaifahamu vizuri?

    Golugwa: Ndio ila sio yote kwa kuisoma.

    Katuga: Kama nilikusikia vyema umezungumza sana ushenzi ushenzi nitakuwa sahihi nikisema wewe ni shahidi wa ushenzi.

    Golugwa: Sio sahihi

    Katuga: Waambie waheshimiwa majaji kabla ya kuwa naibu katibu mkuu ulikuwa katibu mkuu kanda ya kaskazini

    Golugwa: Katibu wa kanda.

    Katuga: Ni kweli ulieleza mahakama kuwa uliandaa taarifa kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa 2024.

    Golugwa: Ni kweli.

    Katuga: Ni kweli kwamba kwenye taarifa yako uliandika maneno makali kwa ushenzi huu ulisema mpaka mshinikize mabadiliko mumshinikize nani?

    Golugwa: Ni kweli na ilikuwa kushinikiza mamlaka husika.

    Katuga: Waambie majaji kama unajua au hujui mtu yoyote akitoa hoja jukumu la kuithibitisha hiyo hoja ni yeye mwenyewe.

    Golugwa: Kwa mujibu wa vifungu vya kisheria sifahamu.

    Katuga: Waambie majaji kama hiyo taarifa ya ushenzi umeileta hapa mahakamani.

    Golugwa: Sijaileta.

    Katuga: Mbali ya kuwa katibu wa kanda ya kaskazini waambie majaji kama ukikuwa na wajibu wwa kupokea taarifa kwa makatibu wengine.

    Golugwa: Nilikuwa ninaratibu na kupokea taarifa kwa makatibu wengine.

    Katuga: Je, ulieleza mahakama kupokea taarifa zao?

    Golugwa: Hapana sikueleza

    Katuga: Waambie majaji wakati ukiwa katibu wa kanda ya kaskazini kama ulikuwa mjumbe wa kamati kuu.

    Golugwa: Sikuwa mjumbe.

    Katuga: Waambie majaji aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema Bwana Mbwowe alitoa tamko akisema hatutakwenda kwenye uchaguzi mwingine wowote bila mabadiliko haya ndio maneno uliyonukuuu?

    Golugwa: Ni kweli

    Katuga: Nitakuwa sahihi nikisema mwenyekiti alionesha kutoridhishwa na mifumo?

    Goligwa: Ni kweli.

    Katuga: Kuna kitu kingine umekisema ukimnukuu mwenyekiti Mbowe Golugwa: Kipi sasa?

    Katuga: Ninasema kuna lingine alisema mbowe zaidi ya haya?

    Golugwa: Hapana.

    Katuga: Hivyo kwa kauli hizi, Mwenyekiti Mbowe aliazimia kwa Chadema kutoshiriki uchaguzi na ilikuwa azimio la kamati kuu.

    Golugwa: Ni kweli.

    Katuga: Kuna sehemu yoyote mwenyekiti alitangaza tofauti na kushiriki uchaguzi tunaenda kuuzuia usifanyike?

    Golugwa: Hayapo.

    Katuga: Waambie majaji kama kuna maneno ya kwenda kuuvuruga uchaguzi yapo hayapo?

    Golugwa: Hayapo

    Katuga: Waambie majaji kama Mbowe alisema tunakwenda kukinukisha vibaya sana.

    Golugwa: Hayapo.

    Katuga: Kwakuwa umekuwa mwema.

    Golugwa: Mimi siwezi kuwa mwema kwako mtu mwenye roho mbaya kama wewe.

    Katuga: Sasa jitu lenye roho mbaya linakuuliza hivi?

    Golugwa: Mtu mwema anakujibu.

    Katuga: je, unajua ni haki kutoshiriki uchaguzi mkuu?

    Gilugwa: Hapana.

    Katuga: Waambie majaji unajua ni haki ya kikatiba kushiriki uchaguzi.

    Golugwa: Ni haki.

    Katuga: Waambie majaji kwa majibu hayo nakiri nitakuwa sahihi nikisema sio haki kumlazimisha asiyetaka kushiriki uchaguzi kushiriki uchaguzi.

    Golugwa: Sio haki kumlazimisha.

    Katuga: Umeelewa kwa mujibubwa katiba gani?

    Golugwa: Katiba ya Jamuhuri ya Muungano.

  11. Shahidi anaendelea kujibu maswali ya upande wa serikali

    Katuga: Ulisema wewe ni mhasibu

    Golugwa:Nimefanya kazi za kihasibu

    Katuga: Wewe sio mhasibu ila ni mtu uliyefanya kazi za kihasibu

    Golugwa: Sahihi Katuga umesema umekuwa mhasibu tangu mwaka 2001 au umekuwa ukifanya kazi za kihasibu tangu 2001 mahakama ichukue lipi?

    Golugwa: Nimekuwa nikifanya kazi za kihasibu tangu 2001.

    Katuga: Kama nimekusikia wewe ndiye mwandishi wa kumbukumbu za vikao vya chama.

    Golugwa: Ndio.

    Katuga; Nitakuwa sahihi nikisema wewe ndiye ulichukuwa na minutes za kikao cha tarehe tatu aprili 2025 Golugwa kile kikao hakikuwa na kuchukua minutes.

    Katuga: Kwa mujibu wa katiba ya Chadema kuna aina ngapi za vikao?

    Golugwa: Kuna aina mbili za vikao

    Katuga: Tuambie ni vikao vipi?

    Golugwa: Vikao vya uchaguzi na utendaji

    Katuga: Ikitokea mtu akasema aina mbili za vikao Chadema ni vya ndani na hadhara nani anasema ukweli

    Golugwa: Wote tuko sawa.

    Katuga: Iambie mahakama vikao vya uchaguzi vinafanana vipi na vikao vya ndani na hadhara.Unaposema vikao vya uchaguzi ulimaanisha nini?

    Golugwa: Nilizungumzia vikao vya uchaguzi wa chama.

    Katuga: Sasa vikao vinatofautianaje?

    Golugwa: Havitofautiani sana.

    Katuga: je, vinafana havifanani?

    Golugwa: Havifanani

    Katuga: Kama nimekusikia umesema hukumbuki masuala ya vikao yako sura ya ngapi?

    Golugwa: Sikumbuki

    Katuga; Nikikuambia viko ibara ya sita utakubaliana na mimi?

    Golugwa: Nikipewa katiba nitasema

    Katuga: Wasomee majaji ibara ya sita ibara ya ndogo ya pili

    Golugwa: Kutakuwa na vikao vya aina nne

    Katuga: Na wewe umewaambia majaji kutakuwa na vikao vya aina mbili sasa majibu yenu na katiba nani anasema ukweli?

    Golugwa: Hapana

    Katuga: kwa hiyo nitakuwa sahihi nikisema hujui katiba ya chama chako

    Golugwa sio kweli.

  12. Golugwa: Mawakili wanawapa watu kesi za uongo

    Lissu

    Katuga: Waambie majaji kama unajua kuulizwa maswali ya dodoso sio suala roho mbaya bali wajibu wa kisheria

    Golugwa: Nafahamu ila kuna mawakili wana roho mbaya wanawapa watu kesi za uongo

    Katuga: Unafahamu kesi jinai ni ushahidi na sio ushabiki?

    Golugwa: Ndio ninafahamu.

    Katuga: Waambie majaji kama ulisema kuna taarifa zako ziko kwemye public domain.

    Golugwa: Nilisema habari ya mawakala ndio ipo kwenye public domain.

    Katuga: Kweli kwamba umekuwa ukizungumza na waandishi wa habari mara kadhaa na ziko kwenye public donain?

    Golugwa: Ni kweli

    Katuga: Ni kweli kwamba wewe ni mjumbe wa kamati kuu ya chadema na ni kutokea lini?

    Golugwa: Ni kweli kuanzia Januari 2025.

    Katuga: Ukiwa mjumbe wa kamati kuu ya chadema mwezi wa nane 2026 kamati kuu ilikaa na kujadili mambo mbalimbali?

    Golugwa: Ni kweli kamati kuu iliketi na kujadili mambo mbalimbali

    Katuga: Waambie majaji kama ni wewe ulitangaza maazimio ya kamati kuu na iko kwenye public domain.

    Golugwa: Ni kweli

    Katuga: Waambie majaji moja ya vitu ulivyo vitangaza ni pamoja na kesi hii

    Golugwa: Ni kweli

    Katuga: Katika kuizungumzia kesi hii ulisema mmekusudia mtamtetea mheshimiwa kwa nguvu zote?

    Golugwa: Sio kweli nilitumia maneno haya viongozi walielekeza muda wao na nguvu katika kumtetea mwenyekiti.

    Katuga: Tofauti ya kuelekeza nguvu na kutetea kwa nguvu kuna tofauti gani?

    Golugwa: Maana yake ni kuweka rasilimali zote kwenye jambo moja.

    Katiga: Nitakuwa sahihi nikisema na wewe ni mmoja wa viongozi hao na umeelekeza nguvu

    Golugwa: Ndio nimeelekeza nguvu hapa.

    Katuga: Tofauti ya kiongozi anayeteuliwa na anayechaguliwa.

    Golugwa: Anayeteuliwa anachaguliwa katikati ya wengi na kuchaguliwa unachaguliwa na wengi

    Katuga: Naibu katibu mkuu Chadema anapatikanaje?

    Golugwa: Anateuliwa.

    Katuga: Anateuliwa na nani?

    Golugwa: Na mwenyekiti wa chama?

    Katuga: Ni mwenyekiti gani wa chama aliyekuteua?

    Golugwa: Na Mh Tundu Lissu

    Katuga: Katibu mkuu wa chama anapatikanaje

    Golugwa: Anateuliwa.

    Katuga: Katibu mkuu wa chama kwa sasa ni nani?

    Golugwa: Anaitwa John Mnyika

    Katuga: Ameteuliwa na nani?

    Golugwa ameteuliwa na mwenyekiti Tundu Lissu

    Katuga: Hii ni kwa mujibu wa nini?

    Golugwa: Katiba ya chama.

    Katuga: Ikitokea mtu akasema yeye uteuzi wake ni wa kamati kuu na sio mwenyekiti atakuwa sahihi?

    Golugwa: Itakuwa sio sahihi.

  13. Siamini ripoti ya Jaji Chande - Shahidi aiambia mahakama

    Ignas: Kwenye zile kanuni za uchaguzi kuna sehemu ulikutana na neno mkwe wa rais

    Golugwa: Hakuna

    Ignas: Umeileza mahakama umewahi kukamatwa na hujawahi kufunguliwa hati ya mashitaka mahakamani

    Golugwa: Ni kweli

    Ignas: Ni kweli baada ya kusikilizwa polisi walikuachia

    Golugwa baada ya mimi kutoa maelezo

    Ignas: Na mara ya pili unasema ulikamatwa tarehe nane mwezi wa kumi na moja napo uliachiwa baada ya kusikilizwa maelezo yako

    Golugwa: Ni kweli

    Ignas: Umeleza elimu yoyote uliyonayo juu ya sheria

    Golugwa: Sina elimu yoyote ya sheria

    Ignas: Sasa umepata wapi ujasiri wa kuieleza mahakama mambo ya kisheria

    Golugwa: Hata Layman anaweza kuongea na yuko mbele yako

    Ignas: Ulieleza kuhusu ripoti za waangalizi ni za mwaka gani

    Golugwa: zote ni za mwaka jana

    Ignas: Wewe ni custodian wa hizo ripoti

    Golugwa: Nilitafuta na kuzihifadhi

    Ignas: Umezileta hapa mahakani

    Golugwa: Hapana

    Ignas: Hizo ripoti zipo kwa lugha gani

    Golugwa: kwa kiingereza

    Ignas: Utakubaliana na mimi wewe sio muandishi wa hizo ripoti

    Golugwa: Ndio mimi sio muandishi wa hizo ripoti

    Ignas: Hao walitoa ripoti kuna siku walikuita uzifasiri toka kingereza kwenda kiswahili

    Golugwa: Kwanini na kwa sababu gani ni tafsiri

    Ignas: Wewe hapa mahakamani umezielezea kwa kiswahili

    Golugwa: Ndio

    Ignas: Utakubaliana na mimi wewe form four ulipata grade gani kingereza

    Golugwa: Sikumbuki

    Ignas: Unatatizo la kumbukumbu

    Golugwa: Ikihitajika ku refresh memory

    Ignas: Je unafahamu mtu akifasiri inaweza kuharibu maana ya ripoti

    Golugwa: Kama mtu akitafsiri vibaya yanaweza kuathiriwa au yasiathiriwe

    Ignas: Umeelaza juu ya uwezo wako kwenye lugha ya kiingereza

    Golugwa: Sio lazima

    Ignas: Unafasiri document za kiingereza

    Golugwa: Kingereza ulipata nini Golugwa C au D

    Ignas: Sasa na D yako unataka kutafsiri ripoti kubwa kama hizi?

    Golugwa: Ina shida gani

    Ignas: Haya tuambie title ya ripoti ya Thabo mbeki kwa kiIngereza ilisemaje

    Golugwa: Kwa kweli sikumbuki

    Ignas: Tuje ile ripoti ya SADC wewe mfasiri inaitwaje

    Golugwa: Kwa kingereza sikumbuki ila inazungumzia

    Iganas: Kwa kingereza bwana wewe si mkalimani

    Golugwa: Sikumbuki

    Ignas: Uliweza kufuatiliwa ripoti ya waangalizi wa Jumuiya ya Afrika mashariki

    Golugwa: Hapana

    Ignas: Tukirudi kwenye hii ripoti ya Jaji Chande uliizungumzia jana swali langu ni kwamba una imani na ripoti hii

    Golugwa: Sina imani nayo

    Ignas: Kwa hiyo hata kile ulicho kieleza jana huna imani nacho licha kuwa kwenye ripoti ya Jaji Chande

    Golugwa: Sikubaliana na wewe nilichokueleza mimi nina imani nacho licha kwamba sina imani na ripoti yote

    Ignas: Inamaana kuna ambavyo vilikupendeza wewe

    Golugwa: Hapana kitu gani hicho kuzungumzia

    Ignas: Hebu turudi kwenye kikao cha watia nia uliongea habari ya unyunyu na makapi kulikuwa na habari ya manukato kwemye kikao chenu cha watia nia

    Golugwa: Haikuwepo - [ ]

    Ignas: Waheshimiwa mimi nimemaliza watafuata wenzangu.

  14. Ignas kwa Golugwa - 'Kwanini malalamishi yenu yalitupiliwa mbali?'

    Ignas: Nimesikia ulikuwa kampeni meneja na hukugombea nafasi yoyote ile

    Golugwa: Ni kweli

    Ignas: Kwa hiyo ulipata hizo taarifa kwa watu wengine

    Golugwa: Kwa kuwa nilikuwa karibu na wagombea nilikua naona kila kitu

    Iganas: Unatambua matokeo ya uchaguzi ngazi ya ubunge 2020 yanapingwa mahakamani na yapi mlishinda

    Golugwa: Kama nilivyosema chaguzi hizi siwezi kukumbuka ni malalamiko mangapi

    Ignas: Je jambo lolote ambalo mliwasilisha mahakamani na mahakama ikaona hoja zenu zina msingi

    Golugwa; Sikumbuki

    Ignas: Unaweza sasa kuiambia hapa kuwa hoja ulizoleta hapa mahakamani hazikuwa na msingi na hivyo zipuuzwe

    Golugwa: Hapana ni hoja za msingi

    Ignas: Kwa kuwa umelamikia swala la madiwani embu tuambie ni kata ngapi malalamiko yenu yalithibitisha ni sahihi

    Golugwa: Kwenye ngazi ya mahakama sina idadi

    Ignas: Utakubaliana nami malalamiko yenu hayakuthibitishwa na mahakama?

    Golugwa: Sio kweli yalikuwa ni ya kweli

    Ignas: Ni mashauri mangapi mliwasilisha mahakamani

    Golugwa: Hakuna

    Ignas: Mahakamani hamkupeleka

    Golugwa: Uchaguzi ni swala la kisiasa

    Ignas: Hebu tuambie ya kwamba ni maneno ya kusikia na kamati za rufaa zilikubali malamiko yao yalikuwa na shida

    Golugwa: Yote yalitupiliwa mbali

    Ignas: Sababu hayakuwa na mashiko

    Golugwa: yalitupiliwa mbali sababu ya uhuni na ushenzi

  15. Mambo ya kisiasa tunamaliza kisiasa - Golugwa

    Maswali ya Dodoso kwa shahidi namba tatu Aman Sam Golugwa

    Ignas: Ni kweli hukujaza wala kuwasilisha fomu za kugombea katika mamlaka husika

    Golugwa: Sikujaza fomu yoyote ya kugombea

    Ignas: Ni kweli kwamba hukuwasilisha fomu

    Golugwa: Ni kweli

    Ignas: Ni kweli kwamba malamiko uliyoleta hapa mahakamani yalikuwa yanahusu wagombea

    Golugwa: Ni kweli

    Ignas: Malamiko uliyosema hapa mahakamani umeyapata toka vyanzo vingine

    Golugwa: Sio kweli

    Ignas: Mtu akiwa na malalamiko anapeleka wapi

    Golugwa: Kwenye mamlaka husika

    Iganas: Inamaana hujui wapi malamiko yanapopelekwa

    Golugwa: Anapaswa kupelekea pale anapogombea na kwenye kamati ya rufaa

    Ignas: Mlishinda mangapi

    Golugwa: Yalitupiwa mbali sababu ya ushenzi niliosema

    Ignas: Mliwasilisha hayo malalamiko yenu mahakamani

    Golugwa: Tuna tambua ila hatukuona haja ya kwenda mahakamani

    Ignas: Inamaana mlirudhika na maamuzi ya kamati za rufa:

    Golugwa: Hapana mambo ya kisiasa tunamaliza kisiasa

  16. Karibu katika matangazo ya moja kwa moja ya kesi ya uhaini ya Tundu Lissu 04.09.2026.

    Tundu Lissu

    Leo tunaendelea na maswali ya dodoso kwa shahidi namba tatu Aman Sam Golugwa ambaye jana alimaliza kutoa ushahidi wake sasa ni zamu ya Jamuhuri kumuhliza maswali.

  17. Golugwa: Lissu hakushiriki kwenye maandalizi ya mkutano wala kuwaita wanahabari

    Lissu

    Lissu: Turudi kwenye Watazamaji walitumia muda wao Kimataifa, watazamaji wote hao walisemaje juu kufunguliwa kwangu kwa kwsi hii ya Uhaini.

    Golugwa: Kwanza walisikitishwa na walisema kesi hii ya uongo na hawakuona mazingira ya Uhaini kwa kile walichokisikia katika maneno aliyoyazungumza Mh Tundu Lissu na hivyo wakataka na kuzisihi mamlaka zimwachilie huru bila masharti yoyote

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji baraza la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa limesemaje juu ya kesi hii?

    Golugwa: Limesema kukamatwa kwangu kwa Lissu haikua halali na kitendo cha kukamatwa kwake kinaminya uhuru na haki ya kujieleza na shtaka alilofunguliwa ni shtaka katili lenye lengo la kumuumiza na hivyo kutaka mamlaka zimwachilie kwa sababu kesi inaonekana ni ya kisiasa.

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kikao cha Mawaziri wa Jumuiya ya Madola kinasemaje juu ya kesi hii.

    Golugwa: Waheshimiwa majaji kikao cha mawaziri kimesema kwanza kesi hii inadhihirisha unyonyaji wa Demokrasia, kesi hii ni ya kisiasa, na ni batili na hivyo Tundu Lissu aachiliwe bila mashart yoyote.

    Lissu: Sasa turudi kwenye mkutano wa tarehe 3 Aprili 2025.

    Kwenye ushahidi wako jana ulisema Mkutano huu uliandaliwa na Sekretariet ya chama kwa wazo la Katibu Mkuu.

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji watu wengine waliohudhuria

    Golugwa: Watu wengine waliohudhuria mkutano huo walikuwamo viongozi wa chama ambao hawakua watia nia na waandishi wa habari walioalikwa.

    Lissu: Wafafanulie waheshimiwa majaji ukisema viongozi wa chama ambao hawakuwa watia nia una maana gani?

    Golugwa: Ninamaanisha walikuwepo viongozi wa Chama kwenye ngazi ya Jimbo, Mkoa na Wilaya.

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kama viongozi wa Chama ni hao tu.

    Golugwa: Waheshimiwa majaji walikuwepo pia viongozi wakuu ambao sio watia nia nikiwemo mimi mwenyewe.

    Lissu: Shahidi waeleze waheshimiwa majaji wote uliowataja walijuaje kuna mkutano?

    Golugwa: Waheshimiwa majaji nianze na viongozi wakuu, mimi ndiye niliyefanya jukumu la kuwapigia simu viongozi wafuatao, Mwenyekiti Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti Bara John Heche, Makamu Mwenyekiti Zanzibar Said Mzee Saidi na Naibu Katibu Mkuu.

    Hawa niliwapigia simu mimi mwenyewe na kuwaambia kuhusiana na uwepo wa mkutano huo. Wengine waliokuwepo ukumbuni walialikwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Chama Brenda Rupia ambaye ni mjumbe wa Sekretariet.

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji wakati yote hayo yanafanyika mimi nilikua wapi?

    Golugwa: Waheshimiwa majaji wakati haya yote yanafanyika Tundu Lissu alikua kwenye Operesheni ya Chama iliyokuwa inaendelea Kanda ya Nyasa ya No Reforms No Elections.

    Lissu: Waeleze Waheshimiwa majaji kama mimi nilishiriki kwa namna yoyote ile.

    Golugwa: Waheshimiwa Majaji Tundu Lissu hakushiriki kuanzia kwenye maandalizi ya kikao hiki, na hata katika kuwasiliana na kutuma mialiko kwa hao watia nia.

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji ushiriki wangu katika kuwaalika waandishi wa habari

    Golugwa :Tundu Lissu hakushiriki katika kuwaalika waandishi wa habari kuja katika mkutano huu

    Lissu: Imedaiwa kwenye Mahakama hii kwamba mimi ndiye niliyeitisha hao watu kwenye mkutano.

    Golugwa: Waheshimiwa majaji hayo madai yatakua ya uongo, ya upotoshaji.Tundu Lissu Hakuhusika.

    Lissu :Waeleze waheshimiwa majaji uwepo wa Waandishi wa Habari katika mkutano huo

    Golugwa: Walikuwepo waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali, wa Television, Magazeti, Online Television pamoja na Redio

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji vyombo vya habari vilivyowalikishwa.

    Golugwa: Kwa kumbukumbu nakumbuka kulikua na Clouds Tv, nakumbuka uwepo wa Jambo Tv, nakumbuka uwepo wa Chanzo TV, ITV na ninakumbuka kuwaona Waandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi.

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji, hao waandishi walialikwa na nani

    Golugwa: Waheshimiwa majaji walialikwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi Brenda Rupia ambaye ni mjumbe wa Sekretariet.

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kwa kumbukumbu zako uwepo wa masharti yoyote waliopewa hao waandishi wa Habari.

    Golugwa: Hapakuwa na masharti yoyote ambayo wamepewa

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kwa kumbukumbu zako uwepo wa maelekezo kutoka kwangu au kwa kiongozi yoyote juu ya waandishi wa habari juu ya namna ya kufanya kazi

    Golugwa: Hapakuwa na maelekezo kutoka kwa Tundu Lissu au kiongozi yoyote yule kwenda kwa Waandishi wa habari kuhusiana na wao kufanya kazi zao.

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji uwepo wa matangzo ya moja kwa moja yaliyofanywa kwenye mkutano huo yaliyofanywa na vyombo vya habari.

    Golugwa: Ni kweli kulikuwa na matangazo ya moja kwa moja

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji vyombo vya habari vilivyorusha matangazo ya moja kwa moja, kama unavikumbuka.

    Golugwa: Kwa kumbukumbu zangu waliorusha matangazo ya moja kwa moja ni Jambo Tv na Chanzo Tv

    Lissu: Inadaiwa mimi ndiye niliyerusha matangazo hayo kwenye Jambo Tv

    Golugwa : Ni uongo, sio kweli huo ni upotoshaji.

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji uhusika wangu kwenye kuchapisha maneno yaliyopo kwenye hati ya mashtka kwenye Jambo Tv.

    Golugwa: Hakuna uhusika wowote kwamba yeye ndiye aliyechapisha maneno hayo kwenye Jambo Tv.

    Lissu: Kwa ufahamu wako maneno haya yalichapishwa na nani kwenye Jambo Tv.

    Golugwa: Maneno hayo yamechapishwa na Mwandishi wa Habari ambaye tulimualika wa Jambo Tv

    Lissu: Kwa hiyo Shahidi hii tuhuma kwamba mimi ndiye niliyechapisha maneno haya unaizungumziaje?

    Golugwa: Hii tuhuma ni uongo ilikua na nia ya kuzorotesha Operesheni iliyokuwa inaendelea hakuchapisha Tundu Lissu.

    Lissu: Inadaiwa kwamba nilichapisha hayo maneno kwenye mtandao wa Jambo Tv nikiwa na nia ya kuitishia Serikali ya Jamhuri ya Muungano, waeleze Waheshimiwa majaji kama kuna maneno Serikali ya Jamhuri ya Muungano

    Golugwa: Nimeyasikia maneno hapo na mimi nimekuwepo kwenye huo mkutano hakuna neno Serikali ya Jamhuri ya Muungano

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji katika hayo maneno uwepo wa neno Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Golugwa: Waheshimiwa majaji hilo neno halipo

    Lissu:Kwa ufahamu wako mtu akisema msimamo huu msimamo huu unaashiria uasi anakua ametenda kosa gani?

    Golugwa: Hakuna kosa lolote ambalo atakuwa ametenda kwa ufahamu wangu.

    Lissu: Kuna maneno yamezungumzwa kwamba tarehe 29 Oktoba vituo vimechomwa moto, tutaumiza watu, sasa katika maneno niliyokusomea waeleze waheshimiwa majaji uwepo wa maneno tutachoma vituo vya mwendokasi.

    Golugwa: Katika maneno niliyosomewa hakuna neno lolote kwamba tutaenda kuchoma vituo vya mwendokasi, hakuna.

    Lissu: Katika maneno niliyokusomea, waeleze waheshimiwa majaji uwepo wa maneno tutachoma vituo vya kupigia kura

    Golugwa: Hakuna maneno hayo.

    Lissu: Waeleze aheshimiwa majaji kwa kumbukumbu zako iwapo ulimsikia Jaji Chande alitaja waliosababisha hivyo vifo.

    Golugwa : Waheshimiwa kwa kumbukumbu zangu sikumbuki iwapo aliwataja waliosababisha vifo.

    Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji juu ya sababu alizozitoa jaji mkuu kuhusu mauaji hayo.

    Golugwa: Kwa kumbukumbu zangu sababu alizozitoa ni pamoja na madai ya Katiba Mpya, masuala ya utekaji na watu kupotea na manung’uniko ya muda mrefu ya wananchi ambayo hayajakua yametatuliwa.

  18. Mahakamani: Shahidi afichua ripoti za SADC na EU

    Tunsu Lissu Mahakamani
    Maelezo ya picha, Mwenyekitiwa CHADEMA akimuuliza shahidi Golugwa maswali ya dodoso.

    Lissu: Sasa shahidi, kati ya waangalizi wote wa uchaguzi uliowataja, walizungumziaje matukio ya mauaji ya wananchi?

    Golugwa: Kwa ujumla, waangalizi walisema kuwa vyombo vya dola, hasa polisi, waliwapiga waandamanaji na kuwazuia waangalizi kutimiza wajibu wao. Pia waliwapiga na kuwanyang’anya vifaa vyao.

    Lissu: Walisema nini kuhusu mauaji ya wananchi?

    Golugwa: Walisema kuwa vyombo vya dola vilihusika katika mauaji ya waandamanaji, na hivyo walitaka kuwe na uwajibikaji kwa mauaji yaliyofanyika.

    Lissu: Uchaguzi huu uliendeshwa na kusimamiwa na chombo gani?

    Golugwa: Uliendeshwa na kusimamiwa na Tume Huru ya Uchaguzi.

    Lissu: Mwenyekiti na watendaji wa tume hiyo wanapatikanaje?

    Golugwa: Wanapatikana kwa kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

    Lissu: Waeleze majaji mkurugenzi wa tume hiyo anapatikanaje.

    Golugwa: Mkurugenzi wa tume hiyo huteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

    Lissu: Waeleze majaji wasimamizi wa uchaguzi wanapatikanaje.

    Golugwa: Ni watumishi wa umma na huteuliwa kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa na mamlaka husika za uchaguzi.

    Lissu: Waeleze majaji maafisa wasimamizi wa vituo vya kupigia kura (presiding officers) wanapatikanaje.

    Golugwa: Wote huteuliwa na Tume Huru ya Uchaguzi.

    Lissu: Waangalizi wote walisemaje kuhusu uchaguzi huo?

    Soma zaidi:

  19. Lissu: SADC na EU Walisemaje Kuhusu Uchaguzi wa 2025?

    Tundu Lissu

    Golugwa: Walisikitishwa na kuzimwa kwa mitandao ya mawasiliano, pamoja na taarifa za mauaji. Pia walieleza kuwa uchaguzi huo uligubikwa na matukio ya utekaji na kupotea kwa watu kabla ya kupigwa kwa kura.

    Lissu: Watazamaji wa Jumuiya ya Madola walisemaje?

    Golugwa: Waheshimiwa Majaji, sikuiona taarifa ya Jumuiya ya Madola, lakini nilisikia kauli ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola.

    Lissu: Kauli hiyo ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola ilisemaje?

    Golugwa: Alisema amesikitishwa na vurugu na mauaji yaliyotokea, na kwamba Jumuiya ya Madola itaendelea kufuatilia kwa karibu tukio hilo.

    Lissu: Katika ushahidi wako wa jana kuhusu uchaguzi, waeleze majaji matokeo ya uchaguzi huo yalivyokuwa.

    Golugwa: Mgombea urais wa CCM alitangazwa kupata kura milioni 31.6, sawa na asilimia 98.6.

    Lissu: Na wagombea wengine walipata kiasi gani?

    Golugwa: Waheshimiwa Majaji, waligawana asilimia 2.4 zilizobaki.

    Lissu: Matokeo ya ubunge yalikuwaje?

    Golugwa: Sifahamu.

    Lissu: Ya udiwani yalikuwaje?

    Golugwa: Sifahamu.

    Lissu: Sasa waeleze majaji kuhusu Wakfu wa Thabo Mbeki. Walisemaje?

    Golugwa: Waheshimiwa Majaji, Wakfu wa Thabo Mbeki ulizungumzia mambo manne:

    • Uchaguzi wa Tanzania ulikuwa chini ya viwango na miongozo ya uchaguzi wa kidemokrasia.
    • Wapiga kura hawakupata uhuru wa kutimiza wajibu wao wa kidemokrasia kutokana na vurugu zilizotokea.
    • Matokeo ya urais na ubunge yaliyotangazwa hayakuwa ya kweli na hayaakisi utashi wa wananchi waliojitokeza kupiga kura.
    • Taarifa yao ilisema kuwa Tanzania haina serikali yenye uhalali, na kwamba serikali iliyopo imejipatia madaraka kwa mabavu na udanganyifu kupitia uchaguzi usio halali.

    Maelezo zaidi:

  20. Mahakamani: Lissu amtaka shahidi kufafanua ripoti za SADC na EU

    .

    Lissu: Waeleze majaji, kwa ufahamu wako, waangalizi wa uchaguzi wa SADC walisema nini kuhusu uchaguzi huo?

    Shahidi: Walisema uchaguzi wa Tanzania umeshindwa kukidhi vigezo vya uchaguzi wa kidemokrasia. Pia kulikuwa na vitisho dhidi ya viongozi wa vyama vya upinzani, hivyo mazingira ya ushindani hayakuwa sawa. Aidha, hakukuwa na uwazi katika mchakato mzima wa uchaguzi. Kulikuwa na udanganyifu katika mchakato wa uchaguzi na vurugu siku ya uchaguzi. Hivyo, uchaguzi wa Tanzania umekosa uhalali wa kuitwa uchaguzi wa kidemokrasia.

    Lissu: Waeleze majaji, watazamaji wa uchaguzi wa Jumuiya ya Ulaya (EU) walisemaje kuhusu uchaguzi huo?

    Shahidi: Watazamaji wa Jumuiya ya Ulaya, kwanza, walisema wamesikitishwa na matukio ya vurugu yaliyotokea siku ya uchaguzi na yaliyosababisha kuvurugika kwa mchakato wa uchaguzi. Pia wamesikitishwa na uharibifu wa mali, kuzimwa kwa mawasiliano ya mtandao, na taarifa za mauaji.

    Soma zaidi: