Iran yakanusha kuitumia Lebanon kama kipengele kikuu cha mazungumzo na Marekani
Rais wa Lebanon Joseph Aoun amesema Iran inatumia taifa lake kama kigezo au kipengele cha majadiliano kati yao na Marekani.
Aoun amesema kwa sasa wanafanyia kazi sera itakayoitenga Lebanon na vita vyoyote vinavyoendelea eneo hilo la Mashariki ya Kati.
Rais huyo alisema “raia wa Lebanon ndiyo wanalipia gharama kubwa ya maslahi ya Iran, na tumechoka na vita kati ya Israel na Hezbollah”
Aoun alitoa onyo kwa Iran kutoingilia taifa lake na kuiambia Hezbollah kuwa njia pekee ya kumaliza vita na Israel ni kupitia diplomasia.
Rais huyo wa Lebanon aliiambia jeshi la Iran IRGC kuwa “hili si taifa lenu, ni letu, siyo jukumu lenu kuingilia taifa letu”
Akijibu mahojiano hayo ambayo rais wa Lebanon alifanya na shirika la habari la CNN, Waziri wa mambo ya kigeni wa Iran, Abbas Araghchi aliandika kwenye mtandao wa X kuwa,
“Kulingana na Aoun ni Iran imekalia kimabavu maeneo ya Lebanon,kuwahamisha robo ya raia wa taifa hilo na kutekeleza mashambulizi, Rais, ikomboe Lebanon kutoka kwa adui wake halisi”
Waziri huyo wa Iran alimwambia rais wa Lebanon kuwa iwapo Iran ingekuwa inaitumia taifa lake kama kipengele kikuu cha majadiliano basi wangekuwa tayari wameafikia makubaliano na Marekani.
Pia unaweza kusoma: