Rais Putin asema haoni maana ya kukutana na Zelensky kuhusu kumaliza vita vya Ukraine

Chanzo cha picha, Reuters
Rais wa Urusi, Vladimir Putin amesema haoni haja ya kukutana na rais wa Ukraine VlodymyrZelesnky, baada ya kiongozi huyo wa Ukraine kutaka kufanya mazungumzo ya ana kwa ana, ili kumaliza vita kati ya mataifa hayo mawili.
Zelensky alikuwa ameandika barua siku ya Alhamisi akitaka kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na Putin akisema “ni vibaya kusubiria” vita hivi vilivyoanza na Urusi kuvamia Ukraine mwaka wa 2022 kuangaziwa ten ana Marekani.
Rais wa Ukraine pia alitaka kuwepo na usitishaji mapigano.
Putin alijibu barua hiyo akisema ni ya “kifedhuli” na kukataa kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na Zelensky na kusisitiza kuwa mazungumzo lazima yafanyike kabla ya usitishaji mapigano.
“Sioni maana ya mkutano huo” Alijibu Putin alipoulizwa iwapo atakubali mwaliko wa Zelensky
Baada ya kuskia jibu la Putin, Zelensky alisema “Putin amechagua vita tena, hataki kumaliza vita, na dunia imesikitishwa na jibu lake”
Pia unaweza kusoma:













