'Tunaishi katika ulimwengu wa ajabu' - asema Trump baada ya jaribio la mauaji dhidi yake

Chanzo cha picha, reu
Tukio la shambulio la risasi kwenye dhdifa ya Waandishi wa White House linaonekana kuwa jaribio la tatu la mauaji dhidi ya Donald Trump, kufuatia matukio ya Butler, Pennsylvania mnamo Julai 2024, na katika klabu yake ya gofu huko Florida mnamo Septemba mwaka huo.
Lakini katika mahojiano na 60 Minutes jana, Trump alisema: "Sikuwa na wasiwasi. Ninaelewa maisha. Tunaishi katika ulimwengu wa ajabu."
Alipoulizwa kuhusu kilichojiri - ambapo JD Vance aliondolewa wa kwanza ukumbini - Trump alisema "haikuwa rahisi" kwa maafisa wa usalama kumuondoa kwenye chumba hicho.
"Nilitaka kuona kinachofanyika.. nilitaka kuona kinachoendelea. Na kufikia wakati huo ndipo tulibaini, labda kuna kitu kibaya kimetokea."
Alipoulizwa kuhusu "kushuka" alipokuwa akiongozwa kutoka ukumbini, Trump alijibu: "Nilianza kutembea nao [maafisa wa usalama]. Niligeuka, nikaanza kutembea, wakasema, 'Tafadhali shuka. Tafadhali shuka chini.'
"Kwa hiyo nilishuka na yule mwanamke wa kwanza akashuka pia."
CBS, mshirika wa habari wa BBC imeona hati iliyoandikwa inayoaminika kuhusishwa na mshukiwa, Cole Allen, ikisema alitaka kuwalenga wanachama wa utawala wa Trump "kutoka ngazi ya juu hadi chini".
Wakati wa mahojiano ya Dakika 60, Trump alikasirishwa na mwandishi wa habari Norah O'Donnell baada ya kuuliza juu ya yaliyomo kwenye dondoo, ambayo ni yalijumuisha maneno kama vile "mnyanyasaji, mbakaji na msaliti".
Alimsuta O'Donnell kwa kumuuliza juu ya dondoo hizo, na kuongeza kuwa "unapaswa kuona aibu kusema hivyo, kwa sababu mimi sihusiki na mambo hayo".
Maelezo zaidi:






