Klabu
kadhaa bado zinamuwania mshambuliaji wa Brazil, Richarlison, mwenye umri wa
miaka 29, baada ya mpango wake wa kuondoka Tottenham na kujiunga na Vasco da
Gama kuvunjika. (UOL - in
Portuguese)
Philippe
Coutinho, aliyewahi kuichezea Brazil, amekubali kutumia miezi mitatu katika
klabu ya Santos. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 34, aliyewahi kucheza
Liverpool na Aston Villa, anatafakari iwapo ataendelea na soka baada ya kuwa
mchezaji huru tangu Februari, alipoondoka Vasco da Gama. (Globo - in
Portuguese)
Manchester
United inamfuatilia kwa karibu beki wa kushoto wa Bournemouth na timu ya taifa
ya Ufaransa, Adrien Truffert, mwenye umri wa miaka 24, ambaye thamani yake
inakadiriwa kuwa pauni milioni 60.(Teamtalk)
Liverpool
bado inamtaka kiungo wa Inter Milan, Aleksandar Stankovic, mwenye umri wa miaka
21, baada ya kuulizia uwezekano wa kumsajili katika dirisha la usajili la
majira ya joto. (Teamtalk)
Crystal
Palace bado haijakata tamaa ya kumsajili beki wa kati wa Brest, Raphael Le
Guen, mwenye umri wa miaka 20, ambaye ilijaribu kumsajili katika dirisha la
usajili lililopita. (Ouest-France
via SportWitness)
Liverpool
bado inamuwania winga wa Ufaransa, Michael Olise, mwenye umri wa miaka 24,
lakini Bayern Munich haina mpango wa kumuuza katika dirisha la usajili la
Januari. (Christian Falk)
Lamine
Camara sasa ameelekeza nguvu zake katika klabu ya Monaco baada ya mpango wa
siku ya mwisho wa usajili wa kiungo huyo wa Senegal, mwenye umri wa miaka 22,
kujiunga na Chelsea kuvunjika. Camara amesema, “Labda fursa nyingine
zitajitokeza.” (ESPN)
Jadon
Sancho hatarajiwi kujiunga na klabu mpya hivi karibuni, huku winga huyo wa
zamani wa England, mwenye umri wa miaka 26, akiendelea kutathmini chaguo zake
baada ya kuondoka Manchester United mwezi Juni. (Football
Insider)
Lazio
na Parma zimejiunga na Everton katika kuonyesha nia ya kumsajili mshambuliaji
wa zamani wa Argentina, Mauro Icardi, mwenye umri wa miaka 33, ambaye ni
mchezaji huru baada ya kuondoka Galatasaray mwishoni mwa msimu uliopita. (Corriere
dello Sport - in Italian)
Malaga inazingatia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa
zamani wa Manchester United na timu ya taifa ya Ufaransa, Anthony Martial,
mwenye umri wa miaka 30, ambaye ni mchezaji huru baada ya kuondoka klabu ya
Monterrey ya Mexico mwezi Juni. (Mundo Deportivo - in Spanish)