Real Madrid wanavutiwa na mlinzi wa Arsenal na Italia Riccardo Calafiori, 24, ambaye awali alicheza chini ya Jose Mourinho huko Roma. (Sky Sports),
Tottenham wanafikiria kumnunua mlinzi wa Juventus na Brazil Gleison Bremer, 29, kuchukua nafasi ya mchezaji wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 28 Cristian Romero katika safu ya ulinzi ya kati. (Tuttosport – In Itali),
Manchester United hawana nia ya kumsajili Romero kutoka Tottenham lakini wanavutiwa na mlinzi wa Newcastle mwenye umri wa miaka 21 Lewis Hall. (TeamTalk),
Mmiliki mwenza wa Man United Sir Jim Ratcliffe yuko tayari kukidhi matakwa ya mshahara ya kiungo wa Nottingham Forest Elliot Anderson, 23, ili kumleta Manchester United. {Mirror)
Manchester City wanasalia kuwa mstari wa mbele kumsajili Anderson licha ya juhudi za United kuwapiku wapinzani wao. (Star – Subscription Required)
Mkufunzi anayekuja Real Madrid Jose Mourinho anamtaka kiungo wa kati wa West Ham na Ureno Mateus Fernandes ambaye pia anavutiwa na Chelsea. (AS – In Spanish)
Manchester United pia wanatafuta dili la kumnunua Fernandes huku West Ham wakimthamini mchezaji huyo kwa takriban £80m, lakini klabu hiyo ya London haina haraka ya kumuuza. (Sky Sports)
Manchester United wanafikiria kumnunua mlinda lango wa Uingereza, 35, Karl Darlow, ambaye mkataba wake unamalizika Leeds msimu huu wa joto, huku mlinda lango wa Uturuki Altay Bayindir, 28, akitarajiwa kuondoka Old Trafford. (Sports Talks)
Fulham wana nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Nigeria Samuel Chukwueze kutoka AC Milan kufuatia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 kuhudumu kwa mkopo wa msimu mzima katika Craven Cottage, lakini wanajaribu kujadili ada ndogo. (Gazzetta dello Sport – In Itali)
Atletico Madrid wana matumaini ya kumshawishi kiungo wa kati wa zamani wa Manchester City Bernando Silva ajiunge nao badala ya Barcelona au Real Madrid kwa sababu wanaweza kumpa Mreno huyo mwenye umri wa miaka 31 muda zaidi wa kucheza. (Marca – In Spanish)
Fulham wanafikiria iwapo wataanzisha kipengele cha kuachiliwa kwa pauni milioni 8 kwa kocha mkuu wa Ipswich, Kieran McKenna, ambaye anaongoza orodha yao ya wagombea kuchukua nafasi ya Marco Silva. (Sports Talk)
Leicester wako kwenye mazungumzo na kocha mkuu wa zamani wa Southampton na Rangers, Russell Martin kuhusu kuchukua mikoba ya klabu hiyo kufuatia kushuka daraja hadi Ligi ya Kwanza. (Leicester Mercury,)